TO JOIN OUR TELEGRAM GROUP CLICK HERE
TANGAZO NAFASI ZA AJIRA KADA MBALIMBALI
Kwa mujibu wa kibali cha ajira mpya Kumb. Na. FA.97/228/01/9 cha tarehe 13/05/2022 Kutoka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo anapenda kuwatangazia Watanzania wote wenye sifa kuomba nafasi ya Ajira mbalimbali kwa masharti ya kudumu.
Mchanganuo wa kazi ni kama ifuatavyo:
1. Katibu Mahususi III – Nafasi 3
1: KAZI NA MAJUKUMU
Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida. Kusaidia kupokea wageni na kuwasikiliza shida zao na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa. Kusaidia kutunza taarifa/Kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za Mikutano na vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika Ofisi unayofanyia kazi na kumualifu Mkuu wake na wakati unaohitajika. Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada/nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo Ofisini. Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi wake. Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa maofisa walio katika